STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 10, 2010

Sam wa Ukweli kuwasindikiza Mapacha Watatu J'3



MSANII anayekuja juu kwenye muziki wa kizazi kipya, Salum Mohammed 'Sam wa Ukweli', anayetamba na kibao cha 'Sina Raha' anatarajia kulisindikiza kundi la muziki wa danis la 'Mapacha Watatu' katika onyesho la 'Usiku wa Sauti ya Kizazi Kipya cha Dansi' linalofanyika keshokutwa.
Onyesho hilo litakalofanyika kwenye ukumbi wa Stereo Bar, Kinondoni jijini Dar es Salaam na Sam wa Ukweli, atakuwepo kulipamba onyesho hilo kwa vibao vyake murua kikiwemo cha 'Sina Raha' kinachotamba kwa sasa nchini.
Akizungumza na MICHARAZO, mratibu wa onyesho hilo, Sauda Mwilima, alisema onyesho hilo ni maalum kwa ajili ya kuwapa burudani mashabiki wa muziki wa dansi kupitia kundi hilo la Mapacha Watatu linaloundwa na waimbaji nyota watatu toka bendi za Africana Stars na Fm Academia.
Waimbaji hao wanaouunda kundi hilo linalotamba na albamu yao ya 'Jasho la Mtu' ni Khalid Chokoraa na Kalala Junior wa Twanga Pepeta pamoja na Jose Mara toka FM Academia.
"Katika kuwapa raha mashabiki wa muziki wanaojiandaa kuuaga mwaka 2010 na kuukaribisha 2011, nimeandaa Usiku wa Sauti ya Kizazi Kipya cha Dansi utakaofanyika Jumatatu ya Desemba 13, ambapo utapambwa na burudani toka kundi la Mapacha Watatu watakaosindikizwa na nyota wa muziki wa kizazi kipya, Sam wa Ukweli," alisema.
Sauda, alisema maandalizi ya onyesho lao yamekamilika kwa asilimia zote na kuwataka mashabiki kukaa mkao wa kula kupata burudani kabambe toka kwa wakali hao.

No comments:

Post a Comment