STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, June 25, 2011

Dialo kutoka Bondeni ana tatu mpya




MSANII aliyewahi kufanya shughuli zake nchini Afrika Kusini, Zakaria Kazi Mkombozi maarufu kama Dialo, akishirikiana na bendi yake binafsi ameachia nyimbo tatu mpya ikiwa ni maandalizi ya kupakua albamu yao ya kwanza.
Akizungumza na mtandao huu, Dialo, alizitaja nyimbo hizo ambazo zimeanza kusambazwa kwenye vituo vya redio kuwa ni 'Sudan Risen' unaozungumzia hali ya kisiasa nchini Sudan, 'Madoda Mpela' uliombwa Kizulu na 'Let Do It'.
Dialo alisema nyimbo hizo ni kati ya nyimbo zitakazokuwa kwenye albamu yao ijayo ambayo bado hawajaipa jina, ila alisema itakuwa na nyimbo 10 zilizopo kwenye miondoko ya Reggae, Afro Pop na Ragga.
"Baada ya kuwa kimya tangu niliporejea nchini kutoka Afrika Kusini, nilipokuwa nafanya shughuli zangu za muziki, nimefanikiwa kuunda bendi ambayo tumeachia kazi tatu mpya ikiwa ni maandalizi ya kupakua albamu yetu ya kwanza," alisema.
Dialo alisema mbali na kuendesha bendi ya muziki, lakini pia ameanzisha klabu ya vijana kwa ajili ya kuwapa elimu ya stadi za maisha na kujiepusha na matumizi ya dawa za kulevya na kujikinga na ukimwi.
Alisema bendi yake ina jumla ya wasanii sita ambao ni yeye Dialo, Bob Chuwa, Dk Today, Alex, Katanga Junior (mdogo wa aliyekuwa mpiga dramu maarufu nchini, Gabby Katanga, ambaye kwa sasa ni marehemu, Yuzo na Amani.
Dialo, aliyewahi kufungwa kwa muda wa miaka mitatu nchini Afrika Kusini kwa kile alichodai kufanyiwa hila na watu aliokuwa akifanya nao kazi ya muziki nchini humo, alisema beni yao inatarajiwa kutumbuiza mjini Moshi siku ya Juni 17 mwaka huu.
Alisema onyesho hilo litafanyika kwenye ukumbi wa Glacian Sports Bar, ambapo mbali na kutambulisha nyimbo zao, lakini pia watapiga nyimbo za magwiji wengine wa muziki duniani kwa staili ya kukopi.
"Tumeanza kufanya maonyesho ambapo Juni 17 tulikuwa nyumbani Moshi, Kilimanjaro kwenye ukumbi wa Glacian Sports Bar," alisema.

No comments:

Post a Comment