STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 26, 2011

Simba yaanza kwa kusuasua Kagame, Ocean View safi



MABINGWA wa kihistoria wa michuano ya Klabu Bingwa kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati, 'Kagame Cup' Simba ya Tanzania jana ilianza kwa kusuasua michuano hiyo baada ya kulazimishwa suluhu na Vital'O ya Burundi, katika pambano la lililofanyika kwenye Uwanja wa Taifa.
Simba inayopewa nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa kutokana na kucheza nyumba na rekodi yake nzuri michuano hiyo inapofanyika Tanzania, imebakiza mechi dhidi ya Zanzibar Ocean View, Etincelles ya Rwanda na wawakilishi wa Eritrea -- Red Sea.
Nafasi nzuri zaidi ya kupata bao kwa Simba ambayo ilianza mchezo na wachezaji wanne wapya ilikuja mwishoni mwa kipindi cha kwanza wakati Haruna Moshi 'Boban' alipopiga mpira wa kwa tik tak uliogonga mwamba wa mabingwa wa Burundi hao kabla ya kuokolewa na mabeki.
Shuti la 'Boban' ambaye hajacheza kwa miaka miwili kutokana na mzozo wa mkataba kati yake na Gefle IF ya Sweden lilikuja kutokana na krosi ya Ulimboka Mwakingwe ambaye kama mpigaji huyo amerudi kikosini baada ya kuachwa msimu uliopita.
Mwakingwe aliuwahi mpira mikononi mwa mlinda mlango wa Vital'O kufuatia shambulizi kali kwenye lango la wapinzani wa Simba hao, pembeni mwa eneo la hatari kabla ya kupiga krosi.
Kikosi cha Simba yenye pointi moja sawa na Vital'O na ambayo bado ina matumaini ya kusonga mbele kutokana na kundi lake kuwa na nafasi tatu za kucheza robo-fainali, kilikuwa pia na mchezaji wa zamani Said Nassoro 'Cholo' na Walulya Derick.
Kocha wa Simba MOses Basena alisema ameshangazwa na matokeo ya kutofungana wakati Simba ilitengeneza nafasi nyingi katika mchezo huo. Na kweli.
Wakati Vital'O ilicheza kwa kujihami zaidi na kushambulia kwa kushitukiza mara nyingi, Simba ilikuwa na mlolongo wa mashambulizi langoni mwa warundi hao.
Kocha wa Vital'O Younde Kagabo alisema ameridhika na sare hiyo kutokana na timu yake kuwa na wachezaji 10 wapya uwanjani.
Katika mchezo wa kwanza mabingwa wa Zanzibar, Zanzibar Ocean View walianza kwa kishindo michuano hiyo baada ya kuilaza Etincelles ya Rwanda kwa mabao 3-2 na hivyo kuongoza kundi hilo la A linalohusisha timu tano.
Michuano hiyo inatarajiwa kuendelea tena leo kwa mechi za kundi B ambapo mabingwa wa soka nchini Tanzania, Simba itakwaruzana na El Merreikh ya Sudan iliyokuja kwenye michuano hiyo baada ya mabingwa wa nchi yao, Al Hilal kujitoa ili ijiandae vema na Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya makundi inayotarajiwa kuanza mwezi ujao.
Mechi ya Yanga na Wasudan hao ambao inakumbusha fainali za michuano hiyo za mwaka 1986 ambapo Yanga ilikomboa mabao mawili dakika mbili za mwisho wa mchezo kupitia Abubakar Salum 'Sure Boy' kabla ya kulazwa kwa mikwaju ya penati na kuliacha kombe liondoke Tanzania, itachezwa kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Pambano jingine la leo ni la kundi C michezo inayochezwa uwanja wa Jamhuri, Morogoro kwa mabingwa watetezi wa michuano hiyo, APR ya Rwanda kuumana na Ports Authority ya Djibout.

No comments:

Post a Comment