STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 26, 2011

Extra Bongo kujitambulisha Morogoro



BAADA ya ziara ya mafanikio kwenye mikoa ya Lindi, Mtwara na Pwani, bendi ya Extra Bongo 'Next Level', inatarajia kuzuru mkoani Morogoro kwa maonyesho maalum matatu ya kuinadi nyimbo mpya ikiwemo 'Watu na Falsafa' uliotungwa na Ramadhan Masanja 'Banzastone' katika miji ya Kilombero, Ifakara na Kilosa.
Ikiwa mkoani Lindi Extra Bongo ilitumbuiza katika ukumbi wa Lindi Oceanic Hoteli, Mtwara katika ukumbi mpya wa Safari Pub na Pwani katika ukumbi wa Maendeleo mjini Utete ambapo maonyesha hayo yalipata wapenzi wengi.
Akizungumza na MICHARAZO, mkurugenzi wa bendi hiyo, Ally Choki alisema kufuatia mafanikio waliopata kwenye mikoa hiyo ya kusini mwa Tanzania, wapenzi wa mkoa wa Morogoro wameitaka bendi ikatumbuize huko.
Alisema, Julai Mosi Extra Bongo itatumbuiza katika ukumbi wa Jamos Centre uliopo Ifakara kabla ya kwenda Kilombero katika ukumbi wa K2 Centre na kisha mjini Kilosa ambako itakuwa katika ukumbi wa Babilon Luxury Centre.
"Tunakwenda Morogoro baada ya kupata mafanikio katika ziara yetu mikoa ya kusini, tunaamini ziara hii inaweza kupanua milango zaidi ya Extra Bongo kupata mialiko ndani na nje ya Dar ili kusaidia wanamuziki kunufaika," alisema.
Chuki alisema hii ni mara ya pili kwa Extra kufanya ziara mkoani Morogoro, lakini alisema awali ilitumbuiza katika ukumbi uliopo mjini na kwamba hatua ya kwenda hadi wilayani ni mwanzo wa bendi yake kutembelea nchi nzima.
Wakati hayo yakiendelea, Choki alisema kabla ya kwenda Morogoro, leo bendi hiyo itafanya vitu vyake katika ukumbi wa Rufika, Tabata Segerea.

No comments:

Post a Comment