STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 26, 2011

Msondo Ngoma wasaka jina la albamu yao



LICHA ya kukamilisha nyimbo zote sita zitakazokuwepo kwenye albamu yao mpya ijayo, uongozi wa bendi ya Msondo Ngoma 'Baba ya Muziki', bado haujajua albamu hiyo mpya iitwe kwa jina gani.
Msondo ambayo leo inatarajiwa kuendelea na makamuzi yao kwenye ukumbi wa TCC-Chang'ombe, Temeke, imesema inaendelea kutafakari waipe jina gani albamu hiyo ijayo.
Msemaji wa bendi hiyo, Rajabu Mhamila 'Super D', alisema wanamuziki wao wanaendelea kuumiza vichwa kutafuta jina litakalobeba albamu hiyo itakayochukua nafasi ya ile ya mwaka juzi ya Huna Shukrani'.
Super D, alisema hata hivyo siku si nyingi mashabiki wao wao watafahamu jina la albamu hiyo ambayo baadhi ya nyimbo zimekuwa zikitambulishwa kwenye maonyesho yao ndani na nje ya jijini la Dar es Salaam.
"Albamu yetu ijayo bado haijafahamika itaitwaje kwa vile wanamuziki wanaendelea kuumiza vichwa kutafuta jina lake, ila nyimbo zote sita zimeshakamilika na kuanza kutambulishwa kwa mashabiki wetu," alisema.
Alizitaja nyimbo za albamu hizo na watunzi wake kwenye mabano kuwa ni 'Lipi Jema' na 'Baba Kibebe' (Eddo Sanga), 'Dawa ya Deni (Isi'haka Katima), 'Suluhu' (Shaaban Dede), 'Nadhiri ya Mapenzi' (Juma Katundu) na 'Kwa Mjomba Hakuna Urithi (Huruka Uvuruge).

No comments:

Post a Comment