STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 26, 2011

Sikinde yabakisha mbili albamu mpya





BENDI kongwe ya muziki wa dansi ya Mlimani Park 'Sikinde' imebakisha nyimbo mbili kabla ya kukamilisha albamu mpya itakayokuwa na nyimbo sita.
Katibu wa bendi hiyo, Hamis Milambo, alisema hadi sasa bendi yao imekamilisha nyimbo nne ambazo zilitarajiwa kutambulishwa jana kwa mashabiki wao katika onyesho maalum la uzinduzi wa vyombo vyao.
Milambo alizitaja nyimbo hizo nne zilizokamilika kuwa ni 'Jinamizi la Talaka', 'Mihangaiko ya Kazi', 'Kinyonga' na 'Deni Nitalipa'.
"Tumekamilisha nyimbo nne ambazo tutazitambulisha kwa mashabiki wetu na mbili za mwisho tayari zimeshaandikwa mashairi ingawa hazijapewa majina yake," alisema Milambo.
Alisema nyimbo hizo za awali zimetungwa na waimbaji wao mahiri akiwemo mkongwe, Hassani Rehani Bitchuka na wengineo.
Tangu ilipopakua albamu ya 'Supu Imetiwa Nazi', Sikinde haijapakua albamu nyingine tena mpya na hivi karibuni iliondokewa na mtunzi na muimbaji wake nguli, Shaaban Dede aliyetua kwa mahasimu wao, Msondo Ngoma ambapo ameshaibuka na nyimbo mbili mpya.
Nyimbo hizo ni 'Suluhu' uliowekwa kwenye albamu mpya ya Msondo na kingine cha 'Vita Dhidi ya Dawa za Kulevya' uliowekwa kiporo kwa albamu ijayo ya bendi hiyo.

No comments:

Post a Comment