STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 26, 2011

Mapacha Wa3 wajikomboa zaidi




BENDI mpya ya muziki wa dansi ya Mapacha Watatu 'Wazee wa Kuchakachua', imendelea kujikwamua kwa kufanikiwa kupata vyombo vipya vya muziki vyenye thamani ya shilingi milioni 36.
Mmoja wa Wakurugenzi wa bendi hiyo, Khalid Chokoraa alisema wamefanikiwa kununua vyombo kwa juhudi zao wenyewe na kuungwa mkono na baadhi ya mashabiki wao.
Chokora alisema, sasa bendi hiyo inatarajia kuzindua vyombo hivyo leo Jumapili katika ukumbi wa Mzalendo Pub, Kijitonyama, jijini Dar es Salaam ambapo wamealikwa watu mbalimbali akiwemo Asha Baraka.
"Tutazindua vyombo vyetu Jumapili ambapo tumewaalika Wakurugenzi wa bendi mbalimbali na wadau wa muziki wa dansi akiwemo Asha Baraka, Ally Choki, Martin Kasyanju, Mama Sakina na wengine wengi," alisema.
Mkurugenzi huyo alisema vyombo hivyo vitaanza kutumika rasmi kwenye onyesho la pamoja na bendi ya Akudo Impact ambalo linatarajiwa kufanyika Julai 2 katika ukumbi wa Vatican Sinza, jijini Dar es Salaam.
Mapacha Watatu ina albamu ya kwanza ya 'Jasho la Mtu' na sasa iko kwenye maandalizi ya albamu ya pili ikiwa imekamilisha nyimbo za 'Tangulia Shambani', 'Sumu ya Mapenzi remix', 'Mtoto wa Paka' na 'Usia wa Babu'.
Bendi hiyo ilianza kama kundi likiwa na vijana watatu ambao ni Khalid Chokoraa, Jose Mara na Kalala Junior lakini wamepiga hatua kwa kuanzisha bendi ambayo ina wanamuziki ya 10.
Baadhi ya wanamuziki hao ni Allen Kisso (solo), Jimmy London (besi), Sele Tumba (tumba), Erasto Mashine (kinanda), Mariam Bessie, Mariam Zidane, Juddy Chakachua, Mariam na Sabrina Pazi ambao wote ni wanenguaji.

No comments:

Post a Comment