STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, July 15, 2011

Hatimaye Sunzu atua Bongo


MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa timu ya Al Hilal ya Sudan, Felex Sunzu ametua nchini mapema leo tayari kufanya mazungumzo na klabu ya Simba ili kuichezea tyimu hiyo kwa msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2011-2012.
Sunzu alitua leo asubuhi akiambatana na mkewe na hadi wakati huu alikuwa akiendelea kufanya mazungumzo na uongozi wa Simba ili kuweza kumwaga wino wa kuichezea klabu hiyo.
Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange Kaburu aliyempokea mshambuliaji huyo aliyeng'ara kwenye mihuano ya Kombe la Chalenji iliyofanyika mwishoni mwa mwaka jana akiichezea Zambia, iliyoalikwa amesema wakati wowote wataweka taarifa juu ya kumnasa rasmi mkali huyo.
Kwenye uwanja wa ndege, Sunzu ambaye alikuwa akitokea mapumzikoni nchini Nigeria, alisema amekuja nchini na kama atapata fursa ya kumalizana na Simba basi mashabiki wa timu hiyo watarajie makubwa kutoka kwake muhimu apewe ushirikiano.
Nyota huyo ambaye ameshindwa kuitumikia Al Hilal kwa kiwango stahiki kiasi cha klabu yake kutaka kumtoa kwa mkopo, alisema anazifahamu Simba na Yanga na anaimani atang'ara nchini kama ilivyo kwa mzambia mwenzake Davis Mwape aliyepo Yanga.
Simba inahaha kusaka mshambuliaji wa kuziba nafasi ya Mbwana Samatta aliyenunuliwa na TP Mazembe, ambayo Sunzu anaonekana kama 'muarubaini'wa tatizo la safu butu ya ushambuliaji ya timu hiyo iliyoshindwa kutwaa taji la Kagame kwa kulazwa na Yanga bao 1-0 katika mechi ya fainali baina yao iliyochezwa Jumapili iliyopita.

No comments:

Post a Comment