STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, July 15, 2011

Msiwaite wafanyakazi wenu wa ndani majina mabaya


WAAJIRI wa wafanyakazi wa majumbani nchini, wameombwa kuachwa kuwaita majina
mabaya watumishi wao, kwa madai kufanya hivyo ni kushusha hadhi na utu wa wafanyakazi hao ambao ni watu muhimu kwao na familia zao kwa ujumla.
Kadhalika wametahadhariwa kuepuka tabia ya kuwaajiri wafanyakazi wenye umri chini ya
miaka 17 kutokana na ukweli umri huo ni mdogo kwa ajira na pia ni kosa kulingana na sheria za kimataifa kuhusu ajira za watoto.
Hayo yalisemwa na wawezeshaji wa semina ya siku moja ya 'Waajiri Makini' iliyoandaliwa na Shirika la kuhudumia Afya na Maendeleo ya Wanawake na Watoto ya Kiota, (KIWOHEDE), walipokuwa wakitoa mafunzo ya kujenga mauhusiano bora kati ya waajiri na wafanyakazi wa majumbani, iliyofanyika katikati ya wiki iliyopita.
Edda Kawala na Stella Mwambenja wote kutoka KIWOHEDE, walisema tabia ya waajiri
kuwaita majina mabaya watumishi wao na kuwanyanyasa au kuwabagua ni jambo baya kwani
linashusha hadhi na utu wa wafanyakazi hao kinyume na sheria na mikataba wa kazi kimataifa.
Wawezeshaji hao walisema ni wajibu waajiri kuishi kwa wema na watumishi wao kwa
kuwafanya kama sehemu ya familia zao badala ya kuwabagua na kunyanyapaa, kitu ambacho sio ubinadamu na kinachochangia uhasama usio na maana baina ya wawili hao.
Pia waliwataka waajiri kuchungua kuajiri wafanyakazi wenye umri mdogo ili wasiweze kunasa kwenye mikono ya sheria inayokataza ajira kwa watoto.
"Mbali na kuchunga umri, pia msiwe mnawabagua wafanyakazi wenu wakati wamekuwa
msaada mkubwa katika majumba yenu kwa kazi wanazowafanyia, muwalipe vema na kwa
wakati kwa vile nao ni wanastahili mahitaji kama watu wengine," alisema Stella.

No comments:

Post a Comment