STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, July 14, 2011

Tanzania yapongezwa kuridhia mkataba wa ILO


SERIKALI ya Tanzania imepongezwa kwa kuwa miongoni mwa nchi zilizopitisha Mkataba wa Kimataifa wa Kutambuliwa kwa Wafanyakazi wa Majumbani, iliuyopitishwa kwenye Mkutano wa 100 wa Shirika la Kazi Duniani (ILO).
Kadhalika Rais Jakaya Kikwete amepongezwa kwa hutuba aliyoisoma kwenye mkutano huo juu ya serikali ya Tanzania kuwatambua wafanyakazi hao kama watumishi halali wanaoostahiki hakio zote wa waajiriwa, akiombwa kuhakikisha utekezaji unafanyika.
Mratibu wa Shirika la Wafanyakazi wa Majumbani Kanda ya Afrika (IUF), Vick Kanyoka, akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam alieleza maazimio ya mkutano wa ILO uliofanyika mwezi uliopita mjini Geneva, Uswisi.
Kanyoka, alisema kitendo cha Tanzania kuwa miongoni mwa nchi zilizopigia kura ya kupitisha mkataba huo wa 189 wa kuwatambua wafanyakazi wa majumbani ni ushindi kwa wafanyakazi wote ambao kabla ya hapo walikuwa wakichukuliwa kama watumwa.
Aliongeza IUF, inaipongeza Tanzania na Rais Jakaya Kikwete aliyehutubia kwenye mkutano huo Juni 15 mwaka huu na kuiomba serikali hiyo itekeleze kwa vitendo mkataba huo ili wafanyakazi wa majumbani kupata haki na kuthaminiwa kama wafanyakazi wengine.
Alisema ingawa sheria ya kuwalinda na kuwatetea wafanyakazi majumbani ipo, lakin i utekelezaji wake umekuwa ni tatizo na ndio maana IUF inaiomba Tanzania kuhakikisha jambo hilo linapata ufanisi ili kuleta usawa miongoni mwa watumishi hao.
"IUF tunaipongeza Tanzania na Rais wake kwa kuridhika kupitishwa kwa mkataba wa 189 wa kutambulika kwa wafanyakazi wa majumbani, uliopitioshwa Juni 16 mwaka huu ambapo ulipitishwa kwa kura 396, huku 16 zikiukataa miongoni mwa mataifa yaliyoukataa likiwa ni Uingereza," alisema Kanyoka.
Mratibu huyo alisema ni kutekelezwa kwa vitendo kwa mkataba huo kutatoa fursa ya waajiri kuwathamini na kuwajali watumishi hao kwa kuingia nao mkataba na kuwalipa haki zao stahiki kma ilivyo kwa watumishi wengine.
Alisisitiza ni muhimu wafanyakazi hao kusaidia kufanikisha uitekelezaji huo kwa kuwa wa kwanza kuhakikisha wanaingia mikataba na makubalino na waajiri wao kabla ya kuanza kazi ili watakapofanyiwa kinyume iwe rahisi kutetewa na kupata haki zao.

Mwisho

No comments:

Post a Comment