STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, July 14, 2011

Bujibu kuchapana na Mtambo wa Gongo


WAKATI michuano ya Ligi ya Kick Boxing iliyotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi huu ikiahirishwa hadi Desemba, mabondia wakongwe wa ngumi za kulipwa nchini, Maneno Osward na Ernest Bujiku wanatarajiwa kupamba ulingoni kupigana.
Maneno Osward maarufu kama Mtambo wa Gongo atapigana na Bujiku katika moja ya mapambano ya ngumi yatakayoshindikiza pambano la Kick Boxing kati ya Amour Zungu wa Zanzibar dhidi ya Mchumia Tumbo litakalofanyika Julai 30 kwenye ukumbi wa DDC Keko, Dar es Salaam.
Kaseba alisema, mbalio na pambano la Osward na Bujiku siku hiyo pia mabondia wa kike, Jamhuri Said wa Tanzania atapimana ubavu na Rukia Kaselete wa Kenya katika pambano jingine la Kick Boxing.
Alisema michezo mingine itakayosindikiza mipambano hiyo ni kati ya Fadhila dhidi Demu wa Kisarawe, Dragon Kaizum atakayepigana na Faza Boy, Idd dhidi ya Dragon Boy, Lion Heart dhidi ya Begeje na michezo mingine ya ngumi za kulipwa.
Kaseba alisema michezo hiyo inafanyika ili kuwapa burudani wakazi wa Dar es Salaam ambao walikuwa wakijiandaa kushuhudia ligi ya Kick Boxing ambayo imeahirishwa hadi Desemba kwa ajili ya kufanya maandalizi ya kutosha.
"Tumeamua kuahirisha ligi ya Kick Boxing hadi Desemba kutoa muda kwa mabondia kujiandaa na kufanya katika kiwango cha kimataifa, hivyo ili kutowanyima raha wadau wa mchezo huo tumeandaa michezo kadhaa ya Kick Boxing na ngumi za kulipwa siku ya Julai 30 itakayofanyika kwenye ukumbi wa DDC Keko," alisema Kaseba.
Alisema Bujiku na Osward kila mmoja kwa sasa yupo katika maandalizi makali ya kuonyeshana umwamba wakikumbushia enzi zao wakitamba kwenye mchezo huo.

Mwisho

No comments:

Post a Comment