STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 25, 2012

Hili Dude la Kitale ni nouma!

MCHEKESHAJI maarufu nchini, Mussa Yusuf 'Kitale' ameachia wimbo mpya uitwao 'Hili Dude' ukiwa miongoni mwa nyimbo anazoziandaa kwa ajili ya albamu ya kwanza. Akizungumza na MICHARAZO, Kitale ambaye amepata umaarufu mkubwa kwa kuigiza kama 'teja', alisema tayari ameshausambaza wimbo huo mpya katika vituo vya radio huku video yake ikiwa katika hatua za mwisho kabla ya kuachiwa. Kitale alisema kibao hicho ni cha pili kwake baada ya awali kufyatua 'Chuma cha Reli' alichokiimba na Gondo Msambaa. "Nimekamilisha dude jipya, linaitwa 'Hili Dude' ambalo limeshaanza kurushwa hewani ikiwa ni utambulisho wa albamu yangu ambayo tayari nyimbo saba kati ya nane zimeshakamilika," alisema. Alisema katika wimbo huo mpya, ameimba kwa kushirikiana na Mide Zo na Corner ambaye pia ndiye prodyuza wa wimbo huo kutoka studio za Kwanza Records ya mjini Morogoro. Msanii huyo alizitaja nyimbo nyingine zitakazokuwa katika albamu hiyo kuwa ni 'Anajifanya Msela' alioimba na Juma Nature, 'Hili Toto' alioimba na Sharo Milionea na Mide Zo, ' Tulianzishe', 'Kinaunau' na 'Chuma cha Reli'. "Wimbo wa mwisho nimeshautunga, ila sijaurekodi kwa sababu bado naendelea kufanya mazungumzo na mmoja wa wasanii kwa ajili ya kuimba nae," alisema. Aliongeza, ameamua kutumbukia kwenye muziki baada ya kuona fani ya uchekeshaji ikiwa haimlipi kwa vile kazi nyingi hufanya chini ya watu ambao ndio hunufaika.

No comments:

Post a Comment