STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 25, 2012

Watanzania zidini kuniombea, tumaini la kupona lipo-Sajuki

NYOTA wa filamu ambaye yupo nchini India kwa matibabu, Juma Kilowoko 'Sajuki' amewataka Watanzania kuzidi kumuombea kwa Mungu ili aweze kupona matatizo yake, akisema wakati akituoa nchini humo kwa matibabu hali yake ilikuwa tete. Akizungumza toka India, Sajuki alisema hali yake ilikuwa mbaya alipofika nchini humo ambapo alipimwa na kukutwa hana damu na huku akiwa kadhoofika kiasi cha kushindwa kufanyiwa chochote. Alisema hata hivyo uangalizi aliopewa katika siku chache zilizopita hali yake imeimarika na sasa anasubiri kupimwa tena kuona kama anaweza kufanyiwa upasuaji kuondoa uvimbe ambao alidai umeongezeka sehemu nyingine ya tumbo lake. "kwa kweli mpaka nazungumza hivi ujue nimeimarika, nilikuwa na hali mbaya hasa baada ya kubainika kuwa kulikuwa na vivimbe vingine vilivyodhoofisha afya yangu na pia nilikuwa na upungufu wa damu, hivyo nikawa katika uangalizi maalum, ila nashukuru mno na ninawaomba Watanzania waniombee," alisema. Sajuki, alisema wakati wowote kuanzia sasa huenda akafanyiwa upasuaji ambao ndio unaoelezwa ni salama ya maisha yake. Wakati akiondoka nchini, Sajuki aliwaliza watu kutokana na kushindwa kutembea mwenyewe na pia alionekana kadhoofu maradufu tofauti na siku za nyuma kabla ya kusafiri kwenda kufanyiwa matibabu nchini humo. Msanii huyo anatibiwa katika hospitali ya Saifee iliyopo Mumbai na sio Apollo kama ilivyokuwa ikiripitiwa awali na vyombo vya habari.

No comments:

Post a Comment