STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, June 2, 2012

'Maafande' wamnyemelea Ngassa

KLABU nne tofauti zimekuwa zikimnyatia mshambuliaji mahiri wa timu ya Moro United, Benedict Ngassa, kwa ajili ya kutaka kumnasa ili wazichezee timu zao katika msimu moya wa Ligi Kuu Tanzania Bara. Akizungumza na MICHARAZO, Ngassa alizitaja klabu hizo zinazomnyemelea kuwa ni JKT Ruvu, Ruvu Shooting, African Lyon na timu iliyopanda daraja ya Prisons ya Mbeya. Ngassa alisema viongozi wa klabu hizo kwa nyakati tofauti wamekuwa wa kiwasiliana nae na kufanya mazungumzo ingawa alikiri bado hajaafikiana nao mpaka sasa. "Licha ya kufuatwa na viongozi wa klabu hizo, bado sijaamua niende wapi, nitaangalia kwanza masilahi," alisema. Aliongeza kuwa, ingawa anafurahia kunyatiwa na timu hizo, lakini roho yake inamuuma kwa timu yake ya Moro United kushuka daraja akielekeza lawama zake kwa wachezaji walioichezea timu hiyo kwa mkopo. Ngassa, alisema wachezaji waliotua katika timu hiyo kwa mkopo toka klabu mbalimbali nyingine za ligi kuu walikuwa wakiihujumu timu yao ambapo licha ya wachezaji halisi wa Moro kujituma na kuifungia mabao, magoli hayo yalikuwa yakirejeshwa kitatanishi. "sio siri tumeshushwa daraja na wachezaji waliokuja Moro kwa mkopo, inauma sana," alisema. Moro United iliyokuwa imerejea tena Ligi Kuu imejikuta ikishuka daraja ikiungana na timu za Villa Squad na Polisi Dodoma kutokana na kujikusanyia pointi chache katika mechi 26 ilizocheza msimu huu ambapo Simba waliibuka mabingwa.

No comments:

Post a Comment