STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, June 2, 2012

Mr Blue, Malaki wachanganywa na Msichana Mzuri

Malaki MSANII anayekuja kwa kasi nchini, Sela Myovela 'Malaki' ameachia ngoma mpya iitwayo 'Msichana Mzuri' aliyoimba akishirikiana na mkali wa R&B, Khery Sameer Rajab maarufu kama Mr Blue au 'Kabaysa'. Akizungumza na MICHARAZO, Malaki aliyewahi kufyatua ngoma nyingine kali iitwao 'Maisha' aliyoimba na mkali wa Bongofleva nchini, Juma Kassim Kiroboto 'Sir Juma Nature' alisema wimbo huo mpya ameurekodia katika studio za Fishcrab chini ya prodyuza matata, Lamar. Malaki alisema wimbo huo uliopo katika miondoko ya R&B ni maalum ya ujio wake mpya chini ya usimamizi wa kaka yake, Mfaiswa Myovela 'Mzee wa FilamuCentral'. "Baada ya kimya kirefu cha miaka kama mitano, nimekuja na ngoma mpya kabisa iitwayo 'Msichana Mzuri' niliyopigwa tafu na Mr Blue, ikifanywa chini ya Lamar wa Fishcrabs Studio," alisema. Alisema, tayari wimbo huo ameshausambaza katika vituo vya redio na kuanza kurushwa hewani, huku mwenyewe nakijipanga kwa ajili ya kuitolea video yake. Aliongeza, lengo lake ni kufyatua albamu hapo baadae ingawa alisema kwa sasa ataendelea kudondosha wimbo mmoja mmoja kwa ajili ya kuweza kujitangaza na kupata shoo zitakazomwezesha kupata fedha za kukamilishia albamu hiyo. Malaki alitumbukia kwenye muziki wa kizazi kipya tangu mwaka 2005 na kutoa kazi yake ya kwanza kabisa akiwa na Juma Nature mwaka 2007 kabla ya kuwa kimya hadi mwaka huu alipotoka na 'ngoma' hiyo mpya.
Mr Blue katika pozi zake.

No comments:

Post a Comment