STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, December 29, 2012

IBF yampongeza Francis Cheka

Bondia Francis Cheka (kushoto) alipokuwa akitunushiana misuli na Chimwemwe kabla ya pambano lao ma juzi mjini Arusha, ambapo Cheka aliibuka mshindi kwa pointi dhidi ya mpinzani wake huyo kutoka Malawi.
SHIRIKISHO la Ngumi la Kimataifa (IBF) limempongeza bingwa mpya wa uzito wa Super Middle wa Bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki yaa Kati, Francis Cheka kufuatia juzi kumtwanga kwa pointi Mmalawi Chiotcha Chimwemwe.
Katika barua yake iliyotumwa kwa Cheka Desemba 28, Mwenyekiti wa Kamati ya Ubingwa wa IBF/USBA, Lindsey Tucker alisema wamefurahishwa na Cheka kutwaa ubingwa na kumtakia kila la heri katika kulishikilia taji hilo.
"Tunachukua fursa hii kukutakia maisha na mafanikio mazuri kama bingwa wa IBF na kumhimiza kuishi kama bingwa". Sehemu ya barua hiyo inasomeka hivyo.
Aidha Tucker amemwagia sifa mpinzani wa Cheka kwa kuonyesha ushupavu na ushindani katika pambano hilo lililofanyika kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha, ambapo alishindwa kwa pointi na mpinzani wake katika pambano hilo lililokuwa kali..
Katika barua hiyo imemkumbusha Cheka kutetea taji lake hilo ndani ya kipindi cha miezi sita.

No comments:

Post a Comment