STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, December 29, 2012

Aziz Gilla atoa ya moyoni, adai hana kinyongo na Coastal Union

Aziz Gilla (kulia) alipokuwa Simba

ALIYEKUWA mshambuliaji wa timu ya Coastal Union ya Tanga, Salim Gilla, ameibuka na kusema hana kinyongo cha kitendo cha kutemwa na klabu hiyo.
Hata hivyo mshambulaji huyo wa zamani wa Simba, aliyeng'ara katika fainali za Kombe la Taifa ya 2009 akiteuliwa kuwa Mchezaji Bora wa mashindano alidai taarifa ya kutemwa kwake na Coastal zilimshtua kupita maelezo.
Akizungumza na MICHARAZO juzi kwa njia ya simu, Gilla aliyeoongoza orodha ya wafungaji ndani ya Coastal kwa msimu uliopita, alisema kama mchezaji anayaheshimu maamuzi yaliyofikiwa na benchi la ufundi la timu hiyo ya kuamua kumtema.
Alisema huenda makocha wa timu hiyo waliomuona sio mchezaji wa mipango yao na kuamua kumtema, hivyo hawezi kupingana na uamuzi hayo zaidi ya kuitakiwa kila la heri timu hiyo katika duru la pili la Ligi Kuu Tanzania Bara.
"Kwa kweli sina kinyongo na maamuzi yaliyofikiwa juu ya kutemwa kwangu kwani ni uamuzi wa kocha, ila nikiri nilishtushwa mno kusikia jina langu ni mioingoni mwa waliotemwa Coastal Union," alisema Gilla.
Mshambuliaji huyo, alisema ni vigumu kuweza kuiwekea kinyongo Coastal kwa vile ni timu ya mkoa wake na ni klabu anayoipenda kwa dhati moyoni.
"Coastal ni timu ya nyumbani, kufanya kwake vema ni sifa kwa mkoa mzima wa Tanga, hivyo siwezi kuichukua zaidi ya kuitakia kila la heri iendeleze moto wa duru la kwanza ili hatimaye itwae ubingwa msimu huu," alisema Gilla.
Coastal Union ilitangaza kuwatema Gilla na wachezaji wenzake kadhaa katika usajili wa dirisha dogo kama njia ya kukiimarisha kikosi chao.
Wengine waliotemwa na mabingwa hao wa zamani wa soka nchini, ni makipa  Juma Mpongo na Jackson Chove, Juma Jabu, Said Sued, Mohamed Issa na Jamal Bachemanga, huku Phillip Maisela, Razak Khalfan, Gerald Lukindo ‘Sipi’ na Shafii Karumani wakitajwa kupelekwa kwa mkopo kwa timu nyingine.

No comments:

Post a Comment