STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, December 29, 2012

Masai Nyota Mbof adai 2012 ulikuwa nomaa!

Masai Nyota Mbof

MCHEKESHAJI anayejitosa kwenye fani ya muziki nchini, Gilliad Severine 'Masai  Nyota Mbofu', amesema mwaka 2012 utakabaki kuwa wa mchungu kwake kutokana na matukio ya kusikikitisha yaliyotokea ndani ya mwaka huo.
Masai anayejiandaa kufyatua wimbo mpya wa 'Masai ya Wapi' akishirikiana na rapa Kalidjo Kitokololo, alisema vifo na kuugua kwa baadhi ya nyota wa sanaa nchini ndiko kunamfanya ashindwe kuusahau mwaka huo.
Alisema kwa kumbukumbu zake tangu Januari mpaka Desemba fani ya sanaa imekuwa  haina nafuu kutokana na kuandamwa na matatizo ikiwemo vifo, ajali na kuugua kwa wasanii wakiwemo waigizaji wa filamu, wachekeshaji na wasanii wa muziki tofauti.
"Kwa kweli pamoja na kumshukuru Mungu kukaribia kuumaliza mwaka 2012, lakini ni vigumu kuusahau kwa jinsi ulivyokuwa mchungu kwangu na wadau wa sanaa  nchini kwa matukio yaliyotokea miezi yote 12," alisema.
Alisema hata hivyo anamuomba Mungu awalinde wasanii na kuufanya mwaka 2013 uwe wa neema, furaha na mafanikio huku akiwasihi wasanii wenzake kumcha Mungu na kuishi kinyenyekevu ili kutomuudhi Muumbaji wao.
"Tunaomba tuuingie mwaka 2013 kwa amani na utulivu na kujipanga upya kwa 2013 ila muhimu tunapaswa kumrudia Mungu ili atupe baraka zake," alisema Masai anayetamba  na wimbo wa 'Rungu na Mukuki'.
Japo Masai hakuyataja matukio yaliyomtia simanzi, ila vifo vya wasanii kama Mzee Kipara, Steven Kanumba, Mlopero, Sharo Milionea, John Stephano, Mariam Khamis na  kuugua kwa akina Vengu, Mzee Small, Sajuki na ajali kadhaa zilizowatokea wasanii   nchini ni kati ya matukio makubwa yaliyojiri ndani ya mwaka 2012.

No comments:

Post a Comment