STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, December 29, 2012

Morris, Machuppa, Kussi waibeba Golden Bush


NYOTA wa zamani wa timu za Simba na Yanga, Herry Morris, Athuman Machuppa na Salum Swedi 'Kussi' leo waling'ara 'mchangani' baada ya kuibeba timu ya Golden Bush kwa kuiwezesha kuinyuka timu ya vijana ya Chuo Kikuu kwa mabao 3-2 katika pambano la kirafiki lililochezwa jijini Dar es Salaam.
Morris aliyewahi pia kuzichezea timu za Prisons Mbeya na Moro United, aliifungia Golden Bush mabao mawili katika pambano hilo maalum la kuagia mwaka 2012 lililochezwa kwenye uwanja wa Chuo Kikuu.
Kivumbi uwanjani kati ya pambano la Chuo Kikuu na Golden Bus Veterani.

Kikosi cha Golden Bush, kikijiandaa kuingia uwanjani kuumana na Chuo Kikuu leo asubuhi kwenyue uwanja wa Chuo Kikuu, Dar es salaam.

Hatari langoni mwa timu ya vijana ya Chuo Kikuu, walipokuwa wakiumana na Golden Bush Veterani asubuhi ya leo kwenye uwanja wa Chuo Kikuu, Dar es Salaam. Golden Bush waliibuka washindi wa mabao 3-2.


Katika pambano hilo lililochezeshwa vema na nyota wa zamani wa Simba na Taifa Stars, Madaraka Seleman 'Mzee wa Kiminyio', Golden ilishuka dimbani na wakali kama Said Swedi 'Pannuci', Athuman Machuppa, Yahya Issa, Steve Marashi, Ben Mwalala, Salum Swedi, Katina Shija na wakali wengine waliotamba Ligi Kuu Tanzania Bara.
Hata hivyo kikosi hicho kilichompoteza 'nahodha' wake, Onesmop Wazir 'Ticotico' aliyeumia dakika ya tisa tu ya mchezo huo ilijikuta ikitanguliwa kufungwa kwa bao 'tamu' lililopachikwa wavuni na nyota wa Chuo Kikuu, Wonder katika dakika ya 13.
Bao hilo lilisawazishwa katika dakika ya 21 na nyota wa mchezo huo, Katina aliyetoa pande murua kwa Morris aliyefunga kwa shuti kali na baadae Omar Mgonja akaiongezea Golden bao la pili dakika ya 38.
Dakika mbili kabla ya mapumziko Chuo Kikuu ilifunga bao la pili na la kusawazisha kupitia tena kwa Wonder baada ya kuwatoka mabeki wa Golden waliokuwa chini ya Salum Kussi, Yahya Issa na Majaliwa na kufanya hadi mapumziko matokeo yawe 2-2.
Kipindi cha pili kilianza kwa Golden kufanya mabadiliko kadhaa ya wachezaji na kuongeza kasi yao ya mashambulizi na kujipatia bao la tatu na la ushindi lililofungwa tena na Morris katika dakika ya 63 kwa mkwaju mkali wa karibu.

Mmoja wa mabeki wa Chuo Kikuu akiondoa mpira langoni mwake walipokuwa wakiumana na Golden Bush na kukubali kipigo cha mabao 3-2.


No comments:

Post a Comment