STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 9, 2013

OMARI OMARI KUZIKWA LEO TEMEKE


MSANII nyota wa miondoko ya Mchiriku, Omari Omari, aliyefariki jana alfajiri anatarajiwa kuzikwa leo saa 7 mchana kwenye makaburi yaliyopo eneo la Temeke Mikoroshini, jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa rafiki ya karibu wa marehemu huyo aliyekuwa akitajwa kama mfalme wa Mnanda King Sapeto, alisema mipango ya mazishi yanaendelea vema na kwamba Omar Omar atazikwa leo mchana.
Sapeto, alisema ndugu na jamaa wa marehemu wanategemea kupata ujumbe mzito kutoka kwa viongozi wa Serikali watakaopishana kwenda kutoa mkono wa faraja kwenye nyumba ya msiba.
Kwa siku za hivi karibuni viongozi wa serikali na vyama mbali mbali vya siasa wamekuwa mstari wa mbele kwa kushiriki bega kwa bega kwenye misiba ya wasanii, hivyo watu wa karibu na Omari Omari wanategemea hali hiyo pia itatokea kwa ndugu yao kipenzi. 
"Hatutegemi ubaguzi wa misiba" anaeleza mmoja wa ndugu wa marehemu.
Omari Omari aliyetamba na wimbo “Kupata Majaaliwa”, alifariki katika hospitali kuu ya Temeke baada ya kuugua ugonjwa wa kifua kikuu.
Msiba wake umekuja siku chache baada ya watanzania kumzika nyota wa filamu, Juma Kilowoko 'Sajuki' aliyefarikia Januari 2, katika hospitali ya Muhimbili alipokuwa amelazwa kwa matatizo ya kiafya.
 
Mwisho

No comments:

Post a Comment