STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 9, 2013

Dogo Muu ‘Siwezi Kushukuru’

Dogo Muu (kulia) akiwa na Dogo Aslay


MSANII chipukizi kutoka kituo cha Mkubwa na Wanae, Muharami Kajonjo 'Dogo Muu' anatarajiwa kuachia kazi mbili tofauti, moja ikiwa 'audio' ya wimbo wake mpya wa 'Nashukuru' na video ya kibao chake kiitwacho 'Siwezi'.
Meneja wa msanii huyo, Said Fella, aliiambia MICHARAZO kuwa wameamua kutoa 'audio' na video kwa lengo la kuwapa burudani mashabiki wa msanii huyo ambaye wanajiopanga ili kumtambulisha rasmi katika ulimwengu wa muziki.
Fella, alisema katika wimbo wa 'Nashukuru'. Dogo Muu ameimba pamoja na msanii nyota aliyetoka kuwania tuzo za Kora Africa, Dogo Aslay.
"Tupo katika maandalizi ya kutoa kazi za msanii wetu mpya, Dogo Muu, tutatoa nyimbo zake mbili katika mfumo wa 'audio' na video, lakini zikiwa tofauti," alisema Fella.
Aliongeza wakati Dogo Muu akijiandaa kujitambulisha kwa mashabiki wa muziki na kazi hizo, kundi la TMK Wanaume Family, nalo limefyatua vibao viwili vipya kimoja kiifahamika kwa jina la 'Tutaonekanaje?
Katika hatua nyingine, alisema pamoja na Dogo Aslay kushindwa katika tuzo za muziki za Kora, lakini fursa ya kuteuliwa kuwania tuzo hiyo kama Msanii Bora Chipukizi, imeonyesha ni namna gani kijana huyo alivyo na kipaji.
"Tunajivunia uteuzi wake, hata kama hatafanikiwa kushinda ikizangatiwa ndio kwanza ameingia kwenye sanaa hii baada ya kukitambua kipaji chake," alisema Fella.

No comments:

Post a Comment