STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 9, 2013

MTANGAZAJI ALIYEPOTEA AKUTWA PORINI AMEKUFA HANA SEHEMU NYETI

Bw. Issa Ngumba.

Mwandishi wa habari wa Radio Kwizera anayefanyia kazi wilayani Kakonko mkoani Kigoma,Bw. Issa Ngumba aliyepotea katika mazingira ya kutatanisha amekutwa amekufa huku akiwa kanyofolewa  sehemu zake za  siri.
 

Taarifa  kutoka Kigoma ambazo mtandao huu  MICHARAZO umezipata jana kuwa, mwili wa mwanahabari  huyo umekutwa nje  kidogo na mkoa  wa Kigoma.
Kamanda  wa  polisi  wa mkoa wa Kigoma Frasser Kishai, amethibitisha  juu ya kutokea kwa  tukio  hilo na kwamba  bado jeshi la polisi linaendelea kufanya uchunguzi.
Mbunge wa  jimbo la Kigoma Zitto Kabwe amenukuliwa kusikitishwa na kifo cha mwandishi huyo na kulitaka jeshi hilo kufanya uchunguzi wa kina juu ya kifo chake.
Kabwe  ameeleza  jinsi  mwanahabari  huyo  alivyokuwa akiifanya kazi yake kwa jamii ya Kigoma kwa ufanisi zaidi na kuwa wakati mwingine yeye kama mbunge alikuwa akizunguka na mwanahabari huyo katika jimbo lake.
" Kweli  nimeguswa   sana na kifo  cha kusikitisha cha mwanahabari huyo nilimfahamu  vema kwa  utendaji kazi wake  ila nawapa  pole sana  waandishi  wote nchini kwa  msiba huu mkubwa .....na zaidi nitapata  kueleza mengi mara baada ya  uchunguzi"
Taarifa za awali  zilizotolewa na  Jeshi la Polisi wilayani Kakonko baada ya  kupotea kwa mwanahabari huyo zilisema kuwa Bw Ngumba alipotea  tangu January 05 mwaka huu majira ya saa 11 jioni ambapo alimuaga mke wake Bi. Rukia Yunus kuwa anakwenda Muhange senta wilayani Kakonko na kwamba hajarudi nyumbani hadi sasa.
Kufuatia tukio hilo jeshi la polisi kwa kushirikiana na wananchi wa Kijiji cha Muhange wanaendelea kumtafuta katika mapori ya kijiji hicho baada ya rafiki zake kueleza kuwa aliwaanga kuwa anakwenda kutafuta dawa msituni.
Bw. Issa Ngumba.
Aidha jeshi la polisi Wilayani Kibondo liliomba kampuni za mitandao ya simu anayotumia Bw Ngumba kusaidia kutambua simu zake zilipotumika kwa mara ya mwisho ili kurahisisha upatikanaji wake.
Akizungumza kwa njia ya simu, Mke wa Bw Issa Ngumba, Bi Rukia Yunus amesema kuwa wananchi walio wengi ambao walikuwa wakimtafuta maporini wamerudi kijiji hapo baada ya kumkosa.

CHANZO:FRANCIS Godwin

No comments:

Post a Comment