STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 30, 2013

Zola D aitoa Swahili Hip Hop kwa mashabiki

Zola D katika pozi



NYOTA wa muziki wa Hip hop nchini, David Mlope 'Zola D', amewafyatulia mashabiki wake albamu yenye nyimbo 21 kama njia ya kuwashukuru kwa namna walivyomuunga mkono tangu ajitose kwenye fani hiyo miaka karibu 20 iliyopita.
Alisema albamu hiyo inayotarajiwa kutoka hivi karibuni imekusanya nyimbo mchanganyiko za zamani na mpya kama njia ya kuwapa burudani mashabiki wake hao sambamba na shukrani zake kwao kwa kumsapoti.
Msanii huyo alisema kwa namna mashabiki wake walivyomuunga mkono tangu alipoibuka mwaka 1995 mpaka sasa hana cha kuwapa zaidi wa kuwatolea albamu hiyo itakayofahamika kama 'Swahili Hip Hop'.
Zola D alisema tayari ameshaanza kuitambulisha albamu hiyo kwa nyimbo zake mpya zinazoendelea kutamba kwenye vituo vya redio na runinga kama 'Coast to Coast' na 'Knockout' aliyouimba akishirikiana na P Funk 'Majani'.
"Sijaona cha kuwapa ahsante mashabiki wangu zaidi ya kuwatolea albamu itakayokuwa na nyimbo mchanganyiko zikiwemo za awali na mpya, ambapo atakayeipata albamu hiyo atasuuzika roho," alisema Zola D.
Alizitaja baadhi ya nyimbo zitakazokuwa katika albamu hiyo ni ya Swahili Hip Hop' ni pamoja na 'Rap Gangster', 'Jana sio Leo', 'Moto wa Tipper', 'Sipati  Mchongo', 'What Going On', 'Hustler King', 'Unde', 'Msela Sana' na 'Rudi'.

No comments:

Post a Comment