STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 30, 2013

EXTRA BONGO, CHID BENZ KUPAGAWISHA MTONI

Waimbaji wa Extra Bongo, Ally Choki na Khadija Kimobitel wakiwajibika jukwaani


BENDI ya Extra Bongo 'Wazee wa Kizigo' inatarajia kufanya onyesho la pamoja na wasanii wa muziki wa kizazi kipya kama njia mojawapo ya kudumisha ushirikiano.
Mkurugenzi wa bendi hiyo Ally Choki alisema onyesho hilo litakalofanyika kesho eneo la Mtoni Kwa Azaz Ally jijini Dar es Salaam, litawashirikisha baadhi ya wasanii kama; Chid Benz, Amin Tundaman na Saynag.
"taratibu huu tuliuanza tangu mwaka jana na tumekuwa tukishirikisha wasanii mbalimbali kwenye maonyesho yetu kama njia mojawapo ya kuimarisha ushirikiano kati ya wanamuziki wa dansi na kizazi kipya," alisema Choki.
Choki alisema baada ya onyesho hilo, Extra Bongo itaendelea na shindano la kila Jumamosi la kucheza mtindo wa 'Kizigo' ambalo linashirikisha mashabiki wa bendi hiyo lililopewa jina la 'Wiki Nne za Zawadi'.
"Sasa tunaingia Jumamosi ya tatu tangu tuanze mashindano haya ambapo mashabiki wamekuwa wakijishindia fedha taslim kuanzia Sh. 150,000 kwa mshindi wa kwanza na Sh. 100,000 kwa mshindi wa pili," alisema.
Alifafanua kuwa shindano limebuniwa kama njia ya kuwashukuru mashabiki wao ambao wamekuwa wakiiunga mkono bendi hiyo tangu ifufuliwe upya miaka mtatu iliyopita ambapo pia mshindi wa tatu hupewa Sh.50,000.
Bendi hiyo kwa sasa inatamba na albamu ya pili ya 'Mtenda Akitendewa' yenye nyimbo za 'Bakutuka', 'Neema', 'Mashuu', 'Fisadi wa Mapenzi' na 'Watu na Falsafa'.


No comments:

Post a Comment