STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 30, 2013

Kikosi cha Azam

AZAM UWANJANI LEO KUIFUKUZIA YANGA KILELENI LIGI KUU BARA

MICHUANO ya Ligi Kuu ya Vodacom inaingia raundi ya 15 leo kwa mechi mbili ambapo Azam iliyo katika nafasi ya pili nyuma ya Yanga itakuwa mwenyeji wa Toto Africans ya Mwanza.
Mechi hiyo itachezwa Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam huku Azam ikisaka ushindi ili kuikaribia Yanga inayoongoza wakati Toto Africans inayonolewa na John Tegete ikitaka kurekebisha makosa ya kupoteza mechi yake iliyopita dhidi ya Oljoro JKT.
Katika mechi hiyo ya Arusha iliyochezwa Jumamosi iliyopita, Toto ililala mabao 3-1 idadi ambayo Azam ilipata kwa kuigaragaza Kagera Sugar inayonolewa na Abdallah KIbadeni.
Uwanja wa Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini Arusha utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Oljoro JKT dhidi ya wageni Kagera Sugar kutoka Bukoba mkoani Kagera itakayochezeshwa na mwamuzi Jacob Adongo wa Musoma.
Ushindi kwa Oljoro JKT yenye pointi 17 utaihakikishia kubaki katika nafasi yake ya nane wakati Kagera Sugar inayofundishwa na kocha mkongwe Abdallah Kibaden utaifanya ipige hatua moja mbele katika msimamo wa ligi.
Ligi itaendelea tena Jumamosi ya wiki hii kwa kuchezwa mechi tatu ambapo vinara Yanga wataumana na Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakiwa na kumbukumbu ya ushindi mnono wa mabao 3-1 mbele ya Prisons ya Mbeya.
Mtibwa katika mechi yao ya kwanza ya duru la pili  ilianza kwa kulazwa nyumbani na Polisi Morogoro, lakini wanajivunia ushindi wa mabao 3-0 iliyoinyuka Yanga katika mchezo wao wa duru la kwanza uliosababisha aliyekuwa kocha wa Yanga, Tom Saintfiet kutimuliwa kazi.

No comments:

Post a Comment