STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 30, 2014

Al Ahly wavuliwa taji Afrika, Vita kama TP Mazembe

Al Ahly waliokuwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa Afrika waliotemeshwa taji jana
MABINGWA watetezi wa Ligi ya Mabingwa Afrika, Al Ahly ya Misri wametemeshwa taji hilo baada ya jana kupokea kipigo cha mabao 3-2 na Al Ahly Benghazi ya Libya.
Watetezi wao walioiondosha Yanga katika hatua ya 32 Bora kwa mikwaju ya penati ilikumbana na kipigo hicho cha aibu nyumbani kwao na kushindwa kuingia hatua ya makundi.
Katika mechi ya kwanza baina ya timu hizo, Al Ahly ya Misri ilifungwa 1-0 na Walibya ugenini na hivyo kung'olewa michuanoni kwa jumla ya mabao 4-2.
Katika mechi nyingine AS Vita ya DR Congo imefuzu hatua ya makundi kuungana na ndugu zao wa TP Mazembe waliofanya hivyo jana licha ya kufungwa 2-0 ugenini na Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini.
Vita ilishinda mechi ya kwanza wiki iliyopita kwa mabao 3-0 na hivcyo kusonga mbele kwa jumla ya mabao 3-2, huku CS Sfaxien ikisonga mbele kwa kushinda nyumbani na ugenini kwa jumla ya mabao 3-0.
Timu hiyo ya Tunisia jana ilishinda nyumbani mabao 2-0, na katika mechi ya wiki iliyopita walishinda ugenini kwa bao 1-0.
Mechi nyingine zinatarajiwa kuchezwa leo Jumapili kuhitimisha idadi ya timu 8 zitakazochuana kwenye makundi kuwania mamilioni ya fedha za CAF.

No comments:

Post a Comment