STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 30, 2014

Mbeya City yainyuka Prisons, Mtibwa yaifumua Coastal 3-1

Mbeya City
Mtibwa Sugar iliyoitungua Coastal kwa mabao 3-1
BAO pekee lililofungwa katika dakika ya pili ya mchezo na Paul Nonga, lilitosha kuipa ushindi muhimu Mbeya City dhidi ya mahasimu wao Prisons na kuipumulia Yanga kisogoni kwenye mbio za kuwania nafasi mbili za juu za Ligi Kuu Tanzania bara msimu huu.
Pambano hilo lililochezwakwenye uwanja wa Sokoine lilikuwa la vuta nikuvute, lakini ni Mbeya waliondeleza ubabe kwa wajelajela hao kwa kuwalaza kwa mara nyingine katika msimu wao wa kwanza wa ligi hiyo baada ya mchezo wa kwanza kuwanyuka 2-0.
Kwa ushindi huo Mbeya City imefikisha pointi 45 moja pungufu na Yanga waliolala 2-1 Mkwakwani Tanga dhidi ya Mgambo JKT.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo iliyochezwa uwanja wa Manungu, Mtibwa Sugar ilipata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya wageni wao Coastal Union.
Mabao ya washindi katika mchezo huo yalifungwa na Jamal Mnyate dakika ya 14 kabla ya Coastal kusawazisha kupitia kwa Mbwana Hamis na Mussa Hassan kuipa uongozi wa 2-1 Mtibwa hadi wakati wa mapumziko.
Kipindi cha pili wenyeji waliongeza bao la tatu dakika nane kabla ya mchezo huo kuisha kupitia kwa Mohammed Mkopi aliyemalizia kazi nzuri ya Mgosi aliyekuwa nyota wa pambano hilo. Mtibwa kwa ushindi huo imefikisha pointi 31.
Nazo timu za Kagera Sugar na Ruvu Shooting zilishindwa kutambiana baada ya kushindwa kufungana katika pambano lililochezwa kwenye uwanja wa Kaitaba, mjini Bukoba, na maafande wa JKT Ruvu wakiwa uwanja wa Chamazi wameichezeshwa kwata Rhino Rangers ya Tabora kwa kuwalaza mabao 3-1 na kuiweka mguu mmoja katika kaburi la kushuka daraja na kurudi Ligi daraja la Kwanza msimu ujao.

No comments:

Post a Comment