STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 30, 2014

Wababe wa Chuoni watupwa Kombe la Shirikisho

http://cdn.pmnewsnigeria.com/wp-content/uploads/2014/03/Bayelsa-United-Team.jpg
Timu ya Bayelsa United ya Nigeria iliyoping'oa How Mine ya Zimbabwe,
WABABE wa Chuoni ya Zanzibar, How Mine ya Zimbabwe imeshindwa kuendelea kutamba katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika baada ya kukwama kwa Bayelsa United ya Nigeria.
Timu hiyo jana ilikubali kipigo cha mabao 2-0 ugenini, baada ya awali kushindwa nyumbani kwao 2-1 na kuwaacha wapinzani wao wakitinga hatua ya makundi ya michuano hiyo ya pili kwa ukubwa Afrika ngazi za klabu.
Katika mechi nyingine wawakilishi pekee wa ukanda wa CECAFA, AS Kigali jana iling'oka kwenye michuano hiyo baada ya kukumbana na kipigo cha mabao 3-0 toka kwa Difaa el Jadida ya Morocco.
Kabla ya kipigo hicho Wanyarwanda hao walishinda nyumbani bao 1-0 na hivyo kutolew akwa jumla ya mabao 3-1 na kurejea Kigali kujipanga upya kwa msimu ujao.
Mabingwa wa zamani wa Afrika, Etoile Sahel ya Tunisia ilifanya kufuru baada ya kuibamiza Super Sport United ya Afrika Kusini nyumbani kwao kwa mabao 4-1, wiki moja baada ya kuitambia 1-0 mjini Tunis.
Etoile imesonga mbele kwa jumla ya mabao 5-1, huku Supersport wakitulia na kuendelea na michuano ya Ligi Kuu nchini mwao.
Mechi nyingine za kukamilisha ratiba ya hatua ya 16 Bora zinachezwa jioni hii.

No comments:

Post a Comment