STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 30, 2014

Monaco yafungwa na kibonde na kuipa nafuu PSG

TIMU ya AS Monaco imetoa mwanya zaidi kwa PSG kunyakua taji la ubingwa wa Ligue 1 kwa mara ya pili mfululizo baada ya usiku wa jana kukubali kipigo cha bao 1-0 ugenini dhidi ya timu ya Evian TG.
Bao la 'jioni' la mkwaju wa penati lililotumbukizwa na  Mkongo Cedric Mongongu, lilitosha kuikwamisha Monaco kuendelea kuipulia japo kwa mbali PSG iliyowaacha kwa pointi 13 wakati ligi ikisaliwa mechi saba kabla ya kukamilishwa kwake.
PSG inaendeelea kuongoza katika msimamo ikiwa na pointi 76, na Monaco ikisaliwa na pointi 63 zote zikiwa zimecheza mechi 31 kila moja.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo zilizochezwa jana Sochaux ilishindwa kutambiana na Olympique Marseille kwa kutoka sare ya 1-1,   Ajaccio  na  Toulouse zilitoksa mabao 2-2, huku Montpellier ikabanwa nyumbani kwake na  Valenciennes kwa kulazimishwa suluhu kama ilivyokuwa kwa pambano la  Nantes na Bordeaux nazo timu za  Reims na Lorient pia zilitoka sare ya 1-1.

No comments:

Post a Comment