STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 30, 2014

Everton yaipumua Arsenal, yaifumua Fulham 3-1

Everton's Steven Naismith celebrates the opening goal at Fulham this afternoonTIMU ya Everton, imeendeleza wimbi lake la ushindi baada ya kupata ushindi mnono wa mabao 3-1 ugenini dhidi ya Fulham na kuitishia Arsenal waliopo juu yao kwa tofauti na pointi nne.
Everton imefikisha jumla ya pointi 60 ikiwa na mchezo mmoja mkononi zaidi ya Arsenal ambayo usiku wa jana ililazimishwa sare ya 1-1 na Manchester City.
Wageni walianza kupata neema dakika sita baada ya kuanza kwa kipindi cha pili baada ya David Stockdale wa Fulham kujifunga kabla ya Ashkan Dejagah kurejesha bao hilo dakika ya 71.
Hata hivyo Everton ikiwa na kiu ya kuwa miongoni mwa timu NNe Bora msimu huu ilicharuka na kuongeza mabao mawili katika dakika ya 79 na 87 kupitia kwa Kevin Mirallas na Steve Naismith na kuzidi kuizika Fulham katika kaburi la kushuka daraja msimu huu.
Fulham imeendelea kusalia mkiani ikiwa na pointi 24 kutokana na kucheza mechi 32 wakati ligi ikiwa imesaliwa na raundi sita kabla ya kukamilisha msimu wake.
Muda mchache baadaye Liverpool watakuwa wakijaribu kutafuta nafasi ya kukwea kileleni itakapoumana na Tottenham Hotspur kwenye uwanja wa Anfield katia mfululizo wa ligi hiyo.

No comments:

Post a Comment