STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 30, 2014

AC Milan yapiga mtu 3-0, Balotelli kama kawa!

MABAO mawili toka kwa Mwanasoka Bora wa zamani wa dunia, Kaka na jingine na 'mtukutu' Mario Balotellu yalitosha kuipa ushindi mnono AC MIlan kwenye uwanja wake wa nyumbani kwa kuifumua Chievo Verona mabao 3-0 katika mfululizo wa Ligi Kuu ya Italia.
Ushindi huo wa pili mfululizo umeifanya Milan kuchupa kutoa nafasi ya 12 hadi ya 9 na kufufua matuamini ya kocha wake Clarence Seedorf.
Balotelli alianza kufunga bao la mapmea dakika ya nne tu ya mchezo huo kumalizia kadi ya Rami kabla ya Kaka kuongeza la pili dakika ya 27  na kuipeleka Milan mapumziko wakiwa mbele kwa 2-0.
Kipindi cha pili Kaka aliongeza jingine katika dakika ya 54 na kuifanya Milan kufikisha jumla ya pointi 42.
Katika mechi nyingine ya ligi iliyochezwa jana Atalanta ikiwa ugenini iliichapa Bologna kwa mabao 2-0.

No comments:

Post a Comment