STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 30, 2014

JKT Ruvu yazidi kudimiza Rhino Rangers

JKT Ruvu
MAAFANDE wa JKT Ruvu chini ya kocha wao Fred Felix 'Minziro' wametoa kipigo kitakatifu kwa Rhino Rangers na kuzidi kuizamisha kwenye tope la kushuka daraja katika mfululizo wa Ligi Kuu Tanzania Bara mchezo uliochezwa uwanja wa Chamazi.
Wenyeji JKT Ruvu ilianza kuandika bao la kwanza dakika za mapema kupitia kwa Idd Mbaga kabla ya Emmanuel Switta kuongeza bao la pili kwa mkwaju wa penati baada ya Sosteness Manyasi kuchezwa rafu na mabeki wa maafande hao wa JWTZ kutoka Tabora na kuifanya Ruvu iendee mapumziko ikiwa 2-0.
Kipindi cha pili kilianza kwa Rhino kupata penati iliyofungwa na Gideon na Ruvu kuongeza bao la gtatu kupitia kwa Samuel Kamutu na kuifanya timu ya Ruvu kufikisha jumla ya pointi 28 na kujiweka kwenye nafasi nzuri zaidi ya kuepuka janga la kushuka daraja msimu huu wakiwa na michezo mitatu mkononi.

No comments:

Post a Comment