STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 30, 2013

BALOTELLI AKUBALI MIAKA MINNE NA NUSU AC MILAN

Balotelli

KLABU ya AC Milan wameafiki dili la kumsajili mshambuliaji Manchester City, Mario Balotelli kwa mkataba wa miaka minne na nusu, mkurugenzi wa klabu hiyo ya Italia, Umberto Gandini, amethibitisha.
Mfumania nyavu huyo wa zamani wa Inter Milan, Balotelli (22) atafanyiwa vipimo vya afya mjini Milan leo (Jumatano) kabla ya kusaini mkataba wake.
Ada ya awali ya uhamisho inaaminika kuwa ni paundi milioni 19 ambayo inasemekana imeshalipwa na huenda ikaongezeka kufikia paundi milioni 22.
Mchezaji huyo mwenye vituko ndani na nje ya dimba, ataondoka Manchester City huku akiwa ameweka gumzo baada ya mwishoni mwa mwaka jana kukwidana na kocha wake, Roberto Mancini wakati wa mazoezi, mbali na matukio mengine ya utata aliyowahi kuyafanya klabu hapo.
Mchezaji huyo

No comments:

Post a Comment