STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, February 25, 2013

SIMBA HATARINI KUPOROMOSHWA ZAIDI

Kikosi cha Coastal Union

WAKATI wakijiandaa na safari yao ya Angola kwa ajili ya pambano la marudiano la Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Libolo, mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba ipo hatarini kuporomoka zaidi kwenye msimamo wa ligi iwapo Coastal Union itashinda pambano lake dhidi ya Ruvu Shooting keshokutwa.
Coastal inatarajiwa kuvaana na Shooting Jumatano kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga, ambapo ushindi wowote itakaopata utaifanya ifikishe poiinti 33 na hivyo kuiengua Simba yenye piointi 31 ambayo haitakuwa dimbani nchini katika ligi hiyo.
Japo Coastal iliyorekebisha makosa kwa kuinyuka Oljoro katika mechi yake iliyopita, isitarajie mteremko kwa Ruvu kwani maafande hao katika mechi zao za duru la pili wameonekana kuimarika zaidi, hivyo huenda ikapata upinzani mkali iwapo watataka kukalia nafasi ya tatu ya msimamo wa ligi hiyo.
Mechi nyingine zitakazochezwa siku hiyo ni pamoja na pambano la kukata na mundu kati ya Yanga na Kagera Sugar ambayo jana ililazimishwa sare ya bao 1-1 na wageni wao African Lyon katika mechi iliyochezwa kwenye uwanja wa Kaitaba.
Katika mechi yao ya awali Yanga ilicharazwa bao 1-0 na Kagera na kuibua hisia kali kwamba kuna baadhi ya wanahabari walitumika kuihujumu timu na kupelekea kutolewa vitisho na kuwapiga marufuku waandishi hao walioambatana na timu hiyo toka Dar kukaa mbali na kambi yao.
Yanga itahitaji ushindi ili kuimarisha nafasi yake ya kukaa kileleni kutokana na kwamba timu inazowafukuza kwa karibu Azam na Simba watakuwa kwenye mechi za kimataifa ugenini mwishoni mwa wiki.
Iwapo Yanga itashinda itafikisha pointi 41 ikiwa michezo sawa na Azam wenye pointi 36 na kuiacha Simba kwa pointi 10 kitu kitakachoiweka katika nafasi nzuri ya kutwaa ubingwa msimu huu.
Michezo mingine kwa siku ya Jumatano kwa mujibu wa ratiba ya ligi hiyo ni Polisi Moro itakayoikaribisha Mgambo JKT uwanja wa Jamhuri Morogoro, JKT RUvu dhidi ya Toto African mechi itakayochezwa uwanja wa Chamazi na 'wababe wa Simba' Mtibwa Sugar watakuwa viwanja vyao vya Manungu Complex kuikaribisha Prisons ya Mbeya.

Msimami kamili wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya mechi za mwishoni mwa wiki ni kama ifuatavyo:



          P W D L GF GA GD Pts
1 Young Africans FC Young Africans 17  12  3 2 33 12 21 39
2 Azam FC Azam 18  11 3 4 31 15 16 36
3 Simba SC Simba 18 8 7 3 26 15 11 31
4 Coastal Union  18 8 6 4 21 16 5 30
5 Kagera Sugar FC Kagera Sugar 18 7 7 4 19 16 3 28
6 Mtibwa Sugar FC Mtibwa Sugar 18 7 6 5 21 18 3 27
7 Ruvu Shooting Stars Ruvu Shooting  16 7 4 5 20 17 3 25
8 JKT Mgambo 17 6 3 8 13 16 -3 21
9 JKT Oljoro 18 5 6 7 19 22 -3 21
10 Prisons-Mbeya 16 4 6 6 10 13 -3 18
11 JKT Ruvu Stars JKT Ruvu Stars 16 4 4 8 14 26 -12 16
12 Toto African Toto African 19 2 8 9 15 28 -13 14
13 African Lyon FC African Lyon 19 3 4 12 13 31 -18 13
14 Polisi Moro 16 2 5 9 8 18 -10 11


No comments:

Post a Comment