STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, March 12, 2013

Golden Bush Fc yazidi kugawa dozi Ligi ya TFF-Kinondoni



LICHA ya kushiriki michuano ya Ligi kwa mara ya kwanza, timu ya soka ya Golden Bush Fc ya Sinza imeendelea kugawa 'dozi' wa wapinzani wao, baada ya juzi kuifumua Makumbusho Talents kwa mabao 3-1 katika mfululizo wa Ligi Daraja la Nne Wilaya ya Kinondoni.
Vijana hao wanaonolewa na nyota wa zamani wa timu za Kagera Sugar na Moro United, Shija Katina huyo ni ushindi wao wa pili mfululizo kwani katika mechi yao ya fungua dimba la michuano hiyo, iliifanyia 'mauaji ya sharubella' timu ya Victoria ya Kijitonyama kwa kuinyuka mabao 6-1.
Ushindi huo umewapa faraja viongozi wa timu hiyo wakiamini ni mwanzo mwema wa ndoto zao za kuwa kufika mbali katika soka la Tanzania wakitamani kufuata nyayo za Azam Fc inayotamba Ligi Kuu Tanzania Bara ikiqwa timu inayomilikiwa na mtu binafsi kuzitetemesha Simba na Yanga na kung'ara kimataifa.

No comments:

Post a Comment