STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, March 14, 2013

Golden Bush kurudiana na watoto wao Jumamosi

Timu ya vijana ya Golden Bush wakiwa na makocha wao ambao baadhi ya wachezaji wa Golden Bush Veterani

 WAKALI wa soka la wazee jijini Dar, Golden Bush Veterani keshokutwa wanatarajia kushuka dimba la Kinesi kumenyana na vijana wao Golden Bush Fc inayoshiriki Ligi Daraja la Nne Wilaya ya Kinondoni.
Pambano hilo ni la marudiano kwa timu hizo baada ya wiki iliyopita vijana hao kuwagaragaza wazee kwa mabao 2-1 katika mechi iliyokuwa na upinzani mkali.
Mlezi wa klabu hizo 'ndugu', Onesmo Waziri 'Ticotico' aliiambia MICHARAZO kwamba mechi hiyo inatarajiwa kuwa ya aina yake kutokana na veterani kupania kulipa kisasi baa ya kunyukwa mechi ya awali.
"Tunatarajiwa kushuka dimbani siku ya jumamosi dhidi ya vijana wetu, Golden Bush Fc ambao walitunyuka mabao 2-1 katika mechi ya awali. Hilo ni pambano litakalosaidia kutuweka vema kabla ya kuvaana na wapinzani wetu, Wahenga Fc," alisema Ticotico.
Ticotico ambaye ni mmoja wa nyota wa timu ya Veterani, alisema pambano lao na Wahenga litachezwa sikukuu ya Pasaka mwishoni mwa mwezi huu.
Timu hizo zimeshakutana mpaka sasa mara tatu, ambapo kila timu imeshinda mechi moja kwa idadi ya mabao 4 na kutoka sare ya bao 1-1 katika pamoja jingine, hivyo mechi ijayo ni ya kukata mzizi wa fitina kuona nani zaidi kati yao.

No comments:

Post a Comment