STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, March 14, 2013

Irene Paul amtoa Kalunde wake hadharani

Micharazomitupu
Msanii Irene Paul 'Brown Eyes' akiwa katika pozi

MSANII anayezidi kukimbiza katika fani ya filamu nchini, Irene Paul amekamilisha filamu yake mpya iitwayo 'Kalunde'.
Akizungumza na MICHARAZO,  Irene alisema filamu hiyo aliyoigiza na wasanii kadhaa nyota aliitarajia kuiachia mtaani kesho Ijumaa baada ya kuikabidhi kwa wasambazaji wake.
Irene alisema hiyo ni kazi yake ya kwanza tangu atumbukie kwenye fani hiyo miaka mitatu iliyopita akiachana na fani ya utangazaji aliyokuwa akiifanya katika vituo viwili kwa nyakati tofauti.
"Nimekamilisha filamu yangu ya kwanza iitwayo 'Kalunde' na ninatarajia kuiachia kwa mashabiki Machi 15," alisema Irene.
Mwanadada huyo aliyecheza filamu kadhaa kama 'Unpredictable', 'Handsome wa Kijiji', I Hate My Birthday, The Shell, Triple L, Fikra Zangu na Shujaa, alisema wakati 'Kalunde' ikiingia mtaani tayari yupo katika maandalizi ya kufyatua filamu nyingine binafsi, ambayo hata hivyo hakupenda kuitaja jina kwa sasa.
"Yaani kwa sasa ni bandika bandua, baada ya Kalunde mashabiki wangu wakae tayari kupata kitu kingine kipya muda si mrefu," alisema Irene.

No comments:

Post a Comment