STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, March 15, 2013

ROBO FAINALI MABINGWA ULAYA WAHISPANIA WATENGANISHWA


  Ratiba ya mechi za robo fainali Ligi ya Mabingwa Ulaya iliyopangwa leo mchana.

MONACO, Ufaransa
RATIBA ya Robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya imetangazwa mchana wa leo huku timu tatu za Hispania na mbili za Ujerumani zikitenganishwa bila kukutana wenyewe kwa wenyewe.
Hispania imeingiza timu tatu katika hatua hiyo ambapo ni mabingwa wa kihistoria wa michuano hiyo Real Madrid, Barcelona na Malaga wakati Ujerumani inafuatia ikiingiza klabu mbili za Bayern Munich na mabingwa watetezi wa nchini hiyo, Borrusia Dortmund.
Kwa mujibu wa atika ratiba hiyo, Malaga ya Hispania itaanzia nyumbani kuumana na Borussia Dortmund, kama itakavyokuwa kwa Real Madrid, iliyopangwa kukipiga na Galatasaray ya Uturuki iliyo na nyota wa zamani wa Galacticos, Wesley Sneijder na Muivoey Coast, Didier Drogba..
PSG ya Ufaransa itakuwa na kibarua kipevu kilichowashinda AC Milan, wakati watakapowaalika FC Barcelona ya Hispania, huku, Bayern Munich ikitarajiwa kukutana uso kwa uso na ‘Kibibi Kizee cah Turin’ Juventus yha Italia.
Mechi za hatua hiyo mkondo wa kwanza zitachezwa Aprili 2 na 3, ambapo mechi kati ya Malaga dhidi ya Dortmund na ile ya Madrid na Galatasaray zitapigwa Jumanne, huku PSG dhidi ya Barca na ile ya Bayern na Juve itapigwa Jumatano.
Michezo ya marudiano zitachezwa kati ya Aprili 9 na 10, kusaka miamba minne itakayocheza nusu fainali ya michuano hiyo, itakayopigwa mwishoni wa mwezi ujao na kurudiana Mei mwanzoni, kusaka tiketi ya fainali Mei 25 kwenye Uwanja wa Wembley. 
Aidha, ratiba ya michuano ya Europa League pia ilipangwa leo katika hafla hiyo, ambapo Chelsea ya England itatoana jasho na Rubin Kazan ya Russia, huku Tottenham Hotspur ya England ikipimana ubabu na FC Basel Uswisi.
Fenerbache ya Uturuki itakuwa na kibarua dhidi yaLazio ya Italia, huku Benfica ya Ureno ikikamuana na Newcastle ya England. Mechi za kwanza robo fainali hii zitapigwa Alhamisi ya Aprili 4 na marudiano yatakuwa Aprili 11.

No comments:

Post a Comment