STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, March 15, 2013

Azam vitani tena Kombe la Shirikisho, TFF yaitakia heri


Na Boniface Wambura

WAWAKILISHI pekee wa Tanzania katika michuano ya Kimataifa, Azam wanatarajiwa kushuka dimbani siku ya Jumapili ugenini kuwakabili wenyeji wao Barrack YC II katika pambano la raundi ya kwanza ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeitakia kila la kheri timu hiyo iweze kufanya vema katika pambano hilo la kwanza litakalochezwa mjini Monravia, Liberia.
Timu hizo zinatarajiwa kurudiana wiki mbili zijazo na tayari Azam wameshatua nchini humo wakiwa na matumaini kibao ya kufanya vema katika mechi hiyo ya kwanza.
TFF imesema wanaungana na watanzania wote hususani mashabiki wa Azam kuiombea heri timu hiyo iweze kuipeperusha vema bendera ya Tanzania.
Azam ilipata nafasi hiyo ya kuendelea mbele kwenye michuano hiyo kwa kuinyuka jumla ya mabao 8-1 Al Nasir Juba ya Suadn Kusini walioumana nao katika mechi ya mzunguko wa awali.
Wawakilishi wengine wa Tanzania waliokuwa wakishiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Simba na Jamhuri Pemba zenyewe ziliondolewa katika raundi ya awali na kuiacha Azam wakiendelea kupeta.

No comments:

Post a Comment