STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, March 5, 2013

TFF yawasilisha barua ya kutaka kuonana na Waziri




NA BONIFACE WAMBURA
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limewasilisha rasmi maombi ya kuonana na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara ili kuzungumzia uamuzi wake wa kutengua usajili wa Katiba ya 2012.
Maombi hayo yaliwasilishwa rasmi Wizarani jana (Machi 4 mwaka huu) ambapo TFF imependekeza kikao hicho kifanyike keshokutwa (Machi 7 mwaka huu) au Machi 13 mwaka huu.
Kamati ya Utendaji ya TFF iliyokutana Machi 2 mwaka huu kujadili tamko ya Waziri kutengua matumizi ya Katiba ya 2012 ndiyo iliyopendekeza kikao hicho kwa lengo la kusikiliza upande wa TFF katika suala hilo.
TFF imeamua kuchukua hatua hiyo kufuatia tamko la serikali kutangaza kuifuta katiba mpya ya shirikisho hilo iliyorekebishwa kwa njia ya waraka na iliyotumika kuwaengua baadhi ya wagombea kwenye uchaguzi wake uliokuwa ufanyike Februari 24 mwaka huu.
Hatua ya serikali imekuwa ikielezwa na wadau kama tisho la Tanzania kuadhibiwa na Shirikisho la Soka Duniani, FIFA linalopinga serikali kuingilia vyama wanachama wake.

No comments:

Post a Comment