STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, April 10, 2013

Filamu ya After Death kutolewa hadharani Mei



FILAMU maalum kwa ajili ya kumuenzi marehemu Steven Kanumba iitwayo 'After Death' iliyozunduliwa kwa kishindo wakati wa hafla ya 'Kanumba Day' inatarajiwa kuachiwa rasmi mwezi ujao.
Kwa mujibu wa waandaaji, filamu hiyo itatoka Mei kwa lengo la kutoa fursa ya kazi mpya ya marehemu Kanumba ya 'Love & Power' iliyozinduliwa pamoja Aprili 7 kwenye viwanja vya Leaders itambe sokoni ikitarajiwa kuachiwa rasmi sokoni Ijumaa hii.
Muongozaji wa filamu hiyo ilitungwa na Jacklyne Wolper, Leah Richard 'Lamata', alisema licha ya mashabiki waliofika Leaders kushuhudia uzinduzi wa filamu hizo kuitaka kuinunua, walikwama kwa vile muda wake wa kuitoa bado.
Lamata alisema mashabiki hao wanapaswa kuwa na subira mpaka mwezi ujao kazi hiyo itakapoachiwa rasmi kulingana na ratiba iliyopo.
"Tunashukuru tumefanikiwa kuwaonjesha ladha na kupokewa vyema kwa filamu hii, lakini mashabiki wanapaswa kusubiri hadi Mei tutakapoiachia rasmi," alisema Lamata.
Filamu hiyo inayoakisi maisha baada ya Kanumba kufariki, imewashirikisha wasanii kadhaa wakiwamo chipukizi waliotamba katika 'This is It' na 'Uncle JJ', Khanifa Daud 'Jennifer' na Othman Njaidi 'Patrick'.
Wengine walioigiza filamu hiyo ni Philemon Lutwazi 'Uncle D', Irene Paul, Patcho Mwamba, Mainda Suka, Shamsa Ford, Jacklyne Wolper na Stanley Msungu.

No comments:

Post a Comment