STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, April 10, 2013

Victoria Sound yakamilisha mpya za albamu yake

 
Mwinjuma Muumin anayeiongoza Victoria Sound

BENDI ya Victoria Sound imekamilisha wimbo mpya wa albamu yao ya kwanza wanayotarajia kuitoa hivi karibuni, pia wakiwa mbioni kurekodi video yao ya pili ya wimbo wa 'Mwisho wa Siku'.
Mkurugenzi wa bendi hiyo, Mwinjuma Muumin 'Kocha wa Dunia' aliiambia MICHARAZO jana kuwa wimbo unaokamilisha albamu umetungwa na muimbaji wao Januari Mavoko haujapewa jina na unaendelea kufanyiwa mazoezi.
Muumin alisema wimbo huo utarekodiwa siku chache zijazo ili kukamilisha jumla ya nyimbo sita na sebene moja kama bonasi kwa mashabiki zitakazokuwa katika albamu ya kwanza.
"Victoria Sound tunaendelea kuufanyia mazoezi wimbo mpya unaokamilisha albamu yetu uliotungwa na Januari Mavoko, ikiwa ni siku chache tangu tutoke kurekodi wimbo wa 'Maisha' uliotungwa na Atosha One," alisema Muumin.
Alisema kuwa Victoria wameamua kurekodi video ya wimbo mmoja mmoja mpaka wamalize zote saba kabla ya uzinduzi baadaye mwaka huu.
Kwa sasa bendi hiyo imerekodi na 'kushuti' video ya wimbo wa 'Shamba la Bibi' ambao mbali na huo pia wamesharekodi nyimbo za 'Utafiti wa Mapenzi' utunzi wa Muumin, 'Mama Bahati' wa Yohana Mbatizaji na 'Maisha'.

No comments:

Post a Comment