STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 23, 2013

Bunge laahirishwa tena, kisa sakata la Mtwara

http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2013/02/8517823001.jpg
Spika wa Bunge, Mhe. Anna Makinda
SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Anna Makinda ameliahirisha tena bunge leo asubuhi ili kupisha kamati ya uongozi ya Bunge iendelee kukutana ili kutoa maamuzi na tamko kuhusu vurugu za Mtwara.
Bunge hilo jana pia liliahirishwa kutokana na sakata hilo ambalo lilijitokeza mapema jana na kusababisha mtu mmoja kufariki dunia na uharibifu mbalimbali kutokea ikiwemo kuchomwa moto nyumba za viongozi wa serikali,chama cha mapinduzi na nyumba ya mwandishi wa habari wa TBC.
Pia mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini umesimamishwa kwa muda mpaka ufumbuzi wa tatizo la vurugu hizo utakapopatiwa suluhisho.

Kesho bajeti ya makadirio ya mapato na matumizi ya Afrika Mashariki itajadiliwa.
 

No comments:

Post a Comment