STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 23, 2013

Shinji Kagawa aipa taji Borussia Dortmund

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg6qnMGGtEdfljwGsrw8rCwj7Az3DybB28VZLR1sfi1mmYGfENc0OAMvIk91kA-UOfpfSkxBVypEs7biZVLGjf9QjGPv1VGFTXYprResinbb3klLzzYOUfYrXyXIVyyW2YP87McxG1lYi4/s1600/Shinji+Kagawa+wallpapers.jpeg
Shinji Kagawa katika uzi wa Manchester United

 

http://ballsybanter.com/wp-content/uploads/2012/06/Cologne-v-Borussia-Dortmund-Shinji-Kagawa-cel_2739644.jpg
Shinji Kagawa alipokuwa akiichezea Borussia Dortmund

 

KIUNGO wa kijapani anayeichezea Manchester United, Shinji Kagawa ametoa turufu yake kwa klabu yake ya zamani Borussia Dortmund kutwaa taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya katika fainali itakayochezwa Jumamosi nchini Uingereza.

Kagawa aliyetua Manchester United msimu uliopita akitokea Dortmund kwa dau la Pauni Milioni 12, alisema anadhani Borussia wataifunga Bayern Munich kwenye fainali za michuano hiyo itakayochezwa katika uwanja wa Wembley.

Pia mchezaji huyo alisema mafanikio iliyopata Dortmund msimu huu kwenye michuano hiyo ya Ulaya licha ya kupoteza ubingwa wa ligi ya Ujerumani, itawachochea Man Utd kufanya vyema kwa msimu ujao wa Ligi hiyo ya Mabingwa Ulaya.

Pamoja na kupoteza taji la nyumbani Dortmund wamekuwa na mafanikio makubwa katika michuano hiyo ya Ulaya licha ya wali kutopewa nafasi kubwa kama klabu nyingine zilizong'olewa au kama ilivyo kwa mahasimu wao Bayern Munich.

Kagawa aliyecheza kwa mafanikio makubwa katika klabu hiyo ya Ujerumani, alisema Dortmund inacheza kwa kujituma na ina wachezaji ambao wanajua wajibu wao uwanjani, licha ya kuimwagia sifa pia Bayern akidai ni timu kubwa na yenye bahati katika soka.

No comments:

Post a Comment