STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 23, 2013

Wanachuo Mwl Nyerere kutembelea yatima

UMOJA wa Wanafunzi Wanachama wa Umoja wa Mataifa Tawi la Mwalimu Nyerere (UNC MNMA) unatarajia kuwatembelea watoto wanaoishi katika mazingira magumu kwenye kituo cha New Hope Familiy kilichopo Ungindoni Maweni, Kigamboni Jijini Dar es Salaam siku ya Jumapili ikiwa ni sehemu ya kuwaaga wanafunzi wanaomaliza chuo hicho hivi karibuni.
Hayo yamebainishwa na Katibu aliyemaliza muda wake hivi karibuni Selemani Msuya wakati akizungumza na mwandishi wa habari hii jijini Dar es Salaam.
Alisema wanachama wa UNC wanaomaliza na wale ambao wanaendelea walikubaliana kwa pamoja juu ya kuwatembelea watoto hao ikiwa ni moja ya malengo yao kushirikiana na jamii iliyokaribu na chuo chao.
Msuya alisema moja ya malengo ya vijana wanachama katika umoja wao wao ni kuhakikisha kuwa wanashirikiana na jamii iliyokaribu nao ikiwa ni kwakushiriki moja kwa moja katika shughuli mbali mbali pamoja na kutoa msaada.
“Sisi vijana wanachama wa UNC kupitia chuo cha Mwalimu Nyerere tumeamua kufanya mahafali ya kuwaaga wenzetu kwa kushiriki chakula  cha mchana na watoto wanaoishi katika mazingira magumu kwani tunaamini kuwa  tutakuwa tumefanya jambo nzuri kwetu na kwa watoto hao,” alisema
Katibu huyo aliyemaliza muda wake ambaye kwa sasa ni mjumbe wa kamati ya utendaji alisema katika ziara hiyo wanatarajia kushiriki chakula cha mchana, kutoa msaada wa vifaa vya shule na kusomea pamoja na kucheza pamoja.
Alisema wana UNC wamejitolea kuchangia kiasi kidogo kulingana na uwezo wao ili kuhakikisha kuwa wanafanya sherehe hiyo ya kuwaagana kwa kushirikiana na watoto ambao wanaishi katika mazingira magumu.
Msuya huyo alisema tukio lingine ambalo litafanyika katika mahafali hayo ni kwa watoto hao ambao wanaishi katika mazingira magumu kuwapatia vyeti wahitimu ambao wanamaliza chuo hivi karibuni.
Katibu huyo ambaye amemaliza muda wake amewataka watu mbalimbali ambao wanatambua changamoto zinazowakabili watoto ambao wanaishi katika mazingira magumu kutoa misaada yao ili waweze kuunganisha na hicho kidogo walichonacho kuwapatia watoto hao.

No comments:

Post a Comment