STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 23, 2013

Polisi Moro waapa kurudi tena Ligi Kuu


Kikosi cha Polisi Moro. Rambow (wa kwanza kushoto mbele)

MSHAMBULIAJI nyota wa timu ya Polisi Moro, Mokili Rambow, amesema licha ya timu yao kushuka daraja, lakini wanaamini watacheza tena Ligi Kuu Tanzania Bara kwa msimu wa 2014-2015.
Rambow, ambaye ni nahodha wa timu hiyo, alisema wamekubali matokeo kwa timu yao kushindwa kuhimili vishindo vya ligi hiyo waliokuwa wakiicheza kwa mara ya kwanza waliposhuka daraja msimu wa 2008-2009 akidai kuwa ilichangiwa na 'ushamba' wa ligi kabla ya kuzinduka duru la pili wakiwa wameshachelewa.
Akizungumza na MICHARAZO, Rambow alisema kushuka kwa timu yao ni pigo na jambo linalowaumiza karibu wadau wote wa klabu hiyo ikizingatiwa waliipigania kuirudisha ligi kuu kwa miaka kadhaa, hata hivyo hawana jinsi zaidi ya kujipanga upya ili kurudi katika ligi hiyo kwa msimu ujao.
Mchezaji huyo ambaye ameifungia mabao kadhaa timu hiyo akishirikiana na wachezaji wenzake, alisema Polisi kwa sasa wanafanya tahmini kabla ya kujiopanga kwa ligi Daraja la Kwanza msimu ujao ambapo aliapa kwamba ni lazima watarejea ligi ya msimu wa 2014-2015.
"Tunajipanga kwa ajili ya kurudi ligi kuu, tunajua ni kazi pevu lakini tutafanhya kila njia kurudi Ligi Kuu kwa kweli tumeumia mno kushuka tulipotoka," alisema Rambow.
Polisi Moro, imemaliza ligi ya msimu huu waliyoicheza baada ya kupanda toka daraja la kwanza, ikiwa na pointi 25 sawa na Toto Africans na kuungana na African Lyon waliotangulia mapema wakiwa na pointi 22 tu.
Katika duru la kwanza Polisi walitolewa nishai na kuambulia pointi nne tu ikiwa na kocha wao maarufu, John Simkoko kabla ya kuachana naye na kumpa jukumu hilo nyota wa zamani wa Yanga, Pan African na Taifa Stars, Mohammed Rishard 'Adolph' aliyeipa jumla ya pointi 21, lakini hazikuwasaidia kuwaokoa wasishuke.

No comments:

Post a Comment