STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 23, 2013

Rio Ferdinand asaini mkataba mpya Man Utd



BEKI mahiri wa Manchester United, Rio Ferdinand amesaini mkataba mpya wa kuendelea kuichezea klabu hiyo na kuzima tetesi kwamba huenda angeachana na klabu hiyo.
Rio mwenye umri wa miaka 34 alinukuliwa akisema kuwa anapenda kuendelea kuichezea timu hiyo na ndiyo maana amesaini mkataba huo mpya wa mwaka mmoja.
"Nimesaini mkataba mpya wa mwaka mmoja," alisema.
Alihoji ni mchezaji gani ambaye asingependa kucheza kwenye klabu kubwa kama Manichester ambayo kila wikiendi zaidi ya watazamaji 74,000 wanakuwepo uwanjani kumshangilia.
Beki huyo aliteua Old Trafford mwaka 2002 akitokea Leeds kwa mkataba uliovunja rekodi wa Pauni Mil 30 na kwa kipindi chote ametwaa mataji 14 tofauti akiwa na kikosi hicho ambacho kinampoteza kocha wake kipenzi na aliyeiweka kwenye kilele cha mafanikio, Sir Alex Ferguson aliyetangaza kustaafu hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment