STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, June 3, 2013

JB, Irene Uwoya waja na Zawadi

Jacob Stephen 'JB'

MUIGIZAJI na mtayarishji hodari wa filamu nchini, Jacob Stephen 'JB' anatarajiwa kuibuka na filamu mpya iitwayo 'Zawadi Yangu'.

Filamu hiyo ambayo imekamilika hivi karibuni ikiwa kwenye foleni kabla ya kuachiwa mtaani ameicheza msanii huyo akiwashirikisha wakali wengine akiwamo mwanadada Irene Uwoya 'Mama Krish', Chuma Suleiman 'Bi Hindu' na Shamsa Ford.

JB anayefahamika pia kwa jina la 'Bonge la Bwana' alisema filamu hiyo ya kijamii inayoonyesha jinsi kinamama wanavyoweza kutawala sehemu kubwa ya ndoa za watoto zao na kudai ni moja ya kazi murua kutoka Jerusalem Films Production kwa namna simulizi lake lilivyo.

"Sijisifu, ila filamu hii mpya ya 'Zawadi Yangu' ni kati ya filamu ambazo nimeiandaa kwa umakini mkubwa na yenye ujumbe maridhawa kwa jamii," alisema JB.

Alisema filamu hiyo itatoka mapema mwezi huu akiwa tayari ameshaanza maandalizi ya 'kupika' kazi nyingine ambayo hata hivyo hakupenda kutaja jina kwa sasa akidai ni mapema mno.

JB aliyewahi kutamba na maigizo kupitia kituo cha ITV akiwa na makundi ya Mambo Hayo na Nyota Ensemble alisema kama ilivyo kwa 'Zawadi Yangu' hata kazi ijayo itakuwa kali na ikishirikisha nyota nchini.

No comments:

Post a Comment