STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, June 3, 2013

Msondo Ngoma yajiandaa kuingioa studio kupakua albamu

 
Baadhi ya wanamuziki wa Msondo Ngoma 'Baba ya Muziki'
BENDI kongwe ya muziki wa dansi nchini, Msondo Ngoma inatarajiwa kuingia studio wiki chache zijazo kurekodi albamu ya kwanza tangu mwaka 2010.

Kwa muda mrefu mashabiki wa Msondo wamekuwa wakiililia albamu mpya tangu ilipotolewa 'Huna Shukrani' miaka mitatu iliyopita na kilio chao kimesikika kwa uongozi wa bendi kwa kuiingiza Msondo studio.

Mmoja wa watunzi wa bendi hiyo, Juma Katundu aliiambia MICHARAZO kuwa wataingia  studio Juni 12.

Katundu ambaye katika albamu hiyo ana wimbo uitwao 'Nadhiri ya Mapenzi', alisema kila kitu kimekaa vyema kwa ajili ya kuanza kazi hiyo ambayo imekuwa ikisubiriwa kwa hamu ya Wanamsondo kwa ujumla kuanzia wanamuziki hadi mashabiki wao.

"Tunatarajiwa kuingia studio Juni 12 kuanza kurekodi nyimbo za albamu yetu ambayo itakuwa na nyimbo sita, mmojawapo ikiwa ni utunzi wangu," alisema.

Alizitaja nyimbo nyingine zitakazorekidiwa kuwa ni 'Baba Kibene' na 'Lipi Jema' za Eddo Sanga, 'Kwa Mjomba Hakuna Mirathi' wa Huruka Uvuruge, 'Dawa ya Deni' na 'Suluhu' wa Shaaban Dede.

Msondo ilitoa albamu ya mwisho mwaka 2010 ambayo ni 'Huna Shukrani' baada ya kuzindua kwa kishindo mwaka mmoja uliotangulia albamu ya 'Kicheko kwa Jirani' iliyokuwa albamu ya kwanza tangu bendi hiyo iondokewe na nyota wake mkubwa, Tx Moshi William.

No comments:

Post a Comment