STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, June 3, 2013

Chelsea yathibitisha Mourinho kutua darajani


Back in town: Jose Mourinho holds his Chelsea shirt after being confirmed as the new Chelsea manager
Kocha Jose Mourinho akiwa na uzi wa Chelsea baada ya kutambulishwa jioni hii

KLABU ya Chelsea imethibitisha  kumjeresha kikosi aliyekuwa kocha wao, Jose Mourinho kwa mkataba wa miaka minne akitokea klabu ya Real Madrid ya Hispania.
Kwa mujibu taarifa zilizotolewa na klabu hiyo jioni hii inasema kuwa wamemalizana na kocha huyo kutoka Ureno na kwamba Mourinho ataanza kazi wiki hii.
Klabu hiyo imemtambulisha rasmi kocha huyo na kukabidhiwa jezi ya klabu hiyo kuthibitisha kuwa sasa ni rasmi karejea nyumbani baada ya kuondoka kwa kuipa mafanikio makubwa ikiwamo kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England mara mbili na lile la Carling Cup mara mbili na Kombe la FA alipotua hapo kwa mara ya kwanza mwaka 2004 hadi 2007 alipoondoka kwenda Inter Milan kabla ya kuchukuliwa Real Madrid.
Hii itakuwa ni mara ya pili kwa Mourinho kuinoa Chelsea ambao wanashikilia taji la Ligi ndogo ya Ulaya baada ya kuinyoa Benfica katika pambano la Fainali lililofanyika Mei 15 mwaka huu, ikiwa ni miezi kadhaa tangu walipolitema taji la Ligi ya Ulaya walilotwaa mwaka jana kwa kuilaza Bayern Munich.

No comments:

Post a Comment